Saturday, December 29, 2012

YANGA SAFARINI KESHO SAA KUMI ALFAJIRI KWENDA UTURUKI NA WACHEZAJI 27

YANGA_MJENGO
>> WACHEZAJI 27 KUPIGA KAMBI MJINI ANTALYA
MABINGWA wa AFRIKA MASHARIKI na KATI, Yanga, kesho Asubuhi wanatarajiwa kuondoka Jijini Dar es Salaam kwa Ndege ya Turkish Airlines kwenda Nchini Uturuki kupiga Kambi ya Mazoezi ya Wiki mbili ikiwa na Wachezaji 27 na Viongozi 7.
Msafara huo mara baada ya kutua Mjini Instanbul utasafiri hadi Mji wa Antalya ulio Kusini Magharibi mwa Uturuki na kufikia Hoteli ya Sueno iliyo ufukweni mwa Bahari ya Mediterranean.
Msafara huo utaongozwa na Mohammed Nyenge, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, na Viongozi wengine ni Kocha Mkuu, Ernest Brandts, Kocha Msaidizi, Fred Felix Minziro, Kocha wa Makipa, Razaki Siwa, Daktari wa Timu, Suphian Juma, Meneja wa Timu, Hafiz Saleh na Afisa Habari, Baraka Kizuguto.
YANGA_UTURUKI
Wachezaji watakaoandaman na Timu hiyo ni:
MAKIPA: Ally Mustafa ‘Barthez’, Said Mohammed na Yusuph Abdul
MABEKI: Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stephano Mwasika na Oscar Joshua.
VIUNGO WAKABAJI: Mbuyu Twite, Nadir Haroub, Ladislaus Mbogo na Kelvin Yondani.
VIUNGO WASHAMBULIAJI: Athumani Iddi, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari, Omega Seme, Saimon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfan na David Luhende.
MASTRAIKA: Didier Kavumbagu, Said Bahanuzi, Jerson Tegete, George Banda na Hamis Kiiza.

No comments:

Post a Comment