Sunday, October 14, 2012

Wayne Rooney ataka Ukepteni wake England uwe wa kudumu

Jumapili, 14 Oktoba 2012 18:29
Chapisha 
WAYNE_ROONEY-KEPTENIStraika wa England Wayne Rooney amesema angependelea itokee Siku awe Kepteni wa kudumu wa Timu ya Taifa ya England baada ya kuiongoza vyema kama Kepteni wa Timu hiyo hapo juzi ilipoitwanga San Marino bao 5-0 huku yeye akipiga bao mbili.
Rooney, Miaka 26, alishika wadhifa huo wa Ukepteni kwa muda kwenye Mechi hiyo baada ya Nahodha wa England, Steven Gerrard, kutokuwepo kufuatia kutumikia Kifungo cha Mechi moja.
Rooney ametamka: “Ukiwa mdogo unaota kuichezea England na ukiichezea kinachofuata ni kutaka kuwa Nahodha!”
Rooney alianza kuichezea England akiwa na Miaka 17 hapo Mwaka 2003 na juzi Ijumaa amefikisha Mechi 77 za kuichezea England.
Bao zake mbili za hiyo Ijumaa zimemfanya afikishe bao 31 akiwa ni wa 5 kwa ufungaji bao nyingi kwa England na sasa amewapiku Nat Lofthouse, Sir Tom Finney na Alan Shearer.
Meneja wa England, Roy Hodgson, amekiri kuwa Rooney anastahili kuwa Kepteni na ipo Siku hilo litatimia.
MATOKEO:
ULAYA-Mechi za Makundi Kombe la Dunia 2014
Ijumaa Oktoba 12
Russia 1 Portugal 0
Finland 1 Georgia 1
Armenia 1 Italy 3
Faroe Islands 1 Sweden 2
Kazakhstan 0 Austria 0
Albania 1 Iceland 2
Czech Republic 3 Malta 1
Liechtenstein 0 Lithuania 2
Turkey 0 Romania 1
Belarus 0 Spain 4
Bulgaria 1 Denmark 1
Moldova 0 Ukraine 0
Slovakia 2 Latvia 1
Estonia 0 Hungary 1
Netherlands 3 Andorra 0
Serbia 0 Belgium 3
Greece 0 Bosnia-Hercegovina 0
Rep of Ireland 1 Germany 6
Wales 2 Scotland 1
England 5 San Marino 0
Luxembourg 0 Israel 6
Macedonia 1 Croatia 2
Switzerland 1 Norway 1
Slovenia 2 Cyprus 1
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumanne Oktoba 16
Albania v Slovenia
Andorra v Estonia
Belarus v Georgia
Belgium v Scotland
Bosnia-Hercegovina v Lithuania
Czech Republic v Bulgaria
Hungary v Turkey
Iceland v Switzerland
Israel v Luxembourg
Latvia v Liechtenstein
Macedonia v Serbia
Portugal v Northern Ireland
Romania v Netherlands
Russia v Azerbaijan
San Marino v Moldova
Slovakia v Greece
Spain v France
Ukraine v Montenegro
2000 Cyprus v Norway
2100 Faroe Islands v Rep of Ireland
2130 Austria v Kazakhstan
2130 Croatia v Wales
2145 Germany v Sweden
2145 Italy v Denmark
2200 Poland v England
FAHAMU:
-ULAYA yapo Makundi 9
-Washindi 9 wa kila Kundi wataingia Fainali moja kwa moja na Washindi wa Pili 8 bora wenye rekodi nzuri dhidi ya Timu zilizomaliza nafasi za Kwanza, Tatu, Nne na Tano kwenye Kundi lao watapelekwa kwenye Droo kupanga Mechi 4 za Mchujo, zitakazochezwa nyumbani na ugenini, ili kupata Timu nne zitakazoingia Fainali.

No comments:

Post a Comment