Friday, September 28, 2012

UWANJANI ULAYA

BPL WIKIENDI=BIGI MECHI: Arsenal v Chelsea, Man United v Spurs!

Alhamisi, 27 Septemba 2012 18:51
Chapisha Toleo la kuchapisha
>>FAHAMU Marefa Mechi zote!
BPL: RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi Septemba 29
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Arsenal v Chelsea
[Saa 11 Jioni]
Everton v Southampton
Fulham v Manchester City
Norwich City v Liverpool
Reading v Newcastle United
Stoke City v Swansea City
Sunderland v Wigan Athletic
[Saa 1 na Nusu Usiku]
Manchester United v Tottenham Hotspur
Jumapili Septemba 30
[Saa 12 Jioni]
Aston Villa v West Bromwich Albion
Jumatatu Oktoba 1
[Saa 4 Usiku]
Queens Park Rangers v West Ham United
======================
Jumamosi Septemba 29 zipo Mechi 8 za Ligi Kuu England [Barclays Premier League, BPL] na kati ya hizo zile zenye mvuto mkubwa, BIGI MECHI, ni ile itayofungua Dimba la Wikiendi itakayochezwa Uwanja wa Emirates kati ya Arsenal na Chelsea na ile itayofunga dimba Siku hiyo hiyo huko Old Trafford kati ya Manchester United na Tottenham Hotspur.
ZIFUATAZO NI DONDOO FUPI kuhusu Mechi hizo:
======================
MSIMAMO Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 5 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea Mechi 5 Pointi 13
2 Man United  12
3 Everton 10
4 WBA  10
5 Arsenal  9
6 Fulham  9
7 Man City  9
8 Tottenham 8
9 West Ham 8
10 Newcastle 8
11 Swansea 7
12 Sunderland Mechi 4 Pointi  4
13 Stoke City 4
14 Aston Villa 4
15 Wigan 4
16 Southampton 3
17 Norwich 3
18 Liverpool 2
19 QPR 2
20 Reading Mechi 4 Pointi 1
=======================
BPL_LOGOArsenal v Chelsea
Hii ni gemu muhimu kwa Arsenal ambao wako nafasi ya 5 na Pointi 4 nyuma ya vinara Chelsea kwenye Msimamo wa Ligi.
Wiki iliyopita Timu hizi zilifunga magoli dakika za mwishoni kwa Arsenal kusawazisha kwa bao la Laurent Koscielny na kutoka 1-1 walipocheza na Mabingwa Manchester City huko Etihad na Chelsea kufunga bao moja kupitia Ashley Cole walipoitoa 1-0 Stoke City.
Hadi sasa, Arsenal na Chelsea ni katika Timu 4 ambazo hazijafungwa kwenye Ligi tangu Msimu uanze na nyingine ni Man City na Sunderland.
Refa: Martin Atkinson
Everton v Southampton
Everton, ambao walianza kwa kuifunga Manchester United bao 1-0, walipwaya kidogo lakini wameshinda Mechi yao ya mwisho kwa kuichapa Swansea bao 3-0  lakini pia wanakutana Southampton ambayo baada ya kuanza vibaya wamezinduka na kuitwanga Aston Villa bao 4-1.
Refa: L Probert
Fulham v Manchester City
Man City wametoka kwenye sare ya 1-1 na Arsenal na wao kama Mabingwa watajiona kama walipoteza mchezo huo lakini Msimu huu Difensi yao inavuja mno na huko Craven Cottage watakutana na Fulham ambayo wao na Man United ndio Timu zilizofunga bao nyingi Msimu huu kwenye Ligi, kila moja ikiwa na bao 12.
Refa: M Halsey
Norwich City v Liverpool
Hii ni Mechi inayozikutanisha Timu zilizo nafasi ya 17, Norwich, na ile ya 18, Liverpool, na kama Liverpool hawaanzi kujirekebisha sasa basi Msimu huu ni balaa kwao.
Refa: M Jones
Reading v Newcastle
Hizi ni Timu mbili ambazo hazitabiriki lakini Newcastle wakiwa na Demba Ba na Papiss Cisse ni hatari ikiwa hiyo itakuwa Siku yao.
Refa: Andrew Marriner
Stoke City v Swansea City
Swansea walianza kwa moto Msimu huu huku mfungaji wao Michu akiwa hashikiki lakini baada ya magoli kumkaukia Swansea wamepigwa Mechi mbili mfululizo kwa jumla ya bao 5-0.
Hii ni Mechi ngumu kutabirika.
Refa: J Moss
Sunderland v Wigan Athletic
Sunderland wamecheza Mechi 4 za Ligi na kupata sare 4.
Hii ni nafasi nzuri kwa Sunderland kupata ushindi dhidi ya Wigan ambayo imefungwa Mechi mbili mfululizo.
Refa: Howard Webb
Manchester United v Tottenham Hotspur
Tangu wafungwe bao 1-0 na Everton katika Mechi yao ya ufunguzi ya Ligi Msimu huu, Man United wameshinda Mechi zao zote 4 zilizofuata na sasa wako nafasi ya pili Pointi moja nyuma ya vinara Chelsea.
Lakini Tottenham walianza vibaya na hatimae kushinda Mechi yao ya mwisho kwa kuifunga QPR bao 2-1.
Refa: C Foy
Aston Villa v West Bromwich Albion
WBA ndio Timu ya maajabu Msimu huu kwani imeanza vizuri Ligi na ipo juu ya Timu kama vile Man City, Arsenal na Tottenham kwenye Msimamo wa Ligi.
Refa: A Taylor
Queens Park Rangers v West Ham United
QPR wako nafasi ya 19 na wanapambana na Timu ngumu iliyo chini ya Meneja Sam Allardyce na Nahodha Kevin Nolan.
Ni Mechi ngumu.
Refa: M Clattenburg

No comments:

Post a Comment