Saturday, September 29, 2012

AVB hahofii Spurs kutua Old Trafford kuivaa Man Utd!

Jumamosi, 29 Septemba 2012 15:25
 
>>SPURS haijashinda OT tangu 1989, akumbushwa kichapo hapo akiwa na Chelsea!!
FERGIE_KAZINIIngawa hali bado tete kwa Meneja Andre Villas-Boas huko Tottenham baada ya kuanza Msimu huu kwa kichapo kwenye Ligi Kuu England na kisha kushinda Mechi mbili na sare mbili na leo inaipeleka Timu yake huko Old Trafford kuivaa Manchester United kwenyre Mechi ya Ligi Kuu England huku mwenyewe akidai Timu yake haitacheza Mchezo wa kujihami.
Akihojiwa kuhusu tuhuma za hivi karibuni toka kwa Meneja wa Manchester City Roberto Mancini ambae alikwaruzana na Meneja wa Aston Villa Paul Lambert na kudai Mameneja wengine huogopa kusema kitu wakiwa Old Trafford, Villas-Boas, mwenye Miaka 34, alisema: “Sina tatizo kuongea chochote nikiwa Old Trafford!”VILLAS-BOAS_N_MANCINI
Alipobanwa aeleza ikiwa Man United wanapendelewa wakicheza Uwanja wao Old Trafford, Villas-Boas alisema: “Ni swali zuri lakini ni swali ambalo Nchi hii huwezi kulijibu. Mwaka jana nilipigwa Faini kubwa kwa kusema kitu kama hiki!”
Leo Andre Villas-Boas anaiongoza Tottenham kucheza Old Trafford ambayo haijashinda Uwanja huo tangu Mwaka 1989 na yeye mwenyewe, akiiongoza Chelsea Msimu uliopita, alijikuta akipigwa 3-1 na Man United.
Lakini mwenyewe amesema: “Tutakwenda huko kucheza Soka la wazi. Hivi ndivyo ninavyopenda na kutaka Timu yangu icheze. Ni ngumu kucheza Old Trafford lakini tunataka kufanya kitu kitakachopa tupa fahari na kufuta hizi takwimu mbaya!”
Akielezea muda wake mfupi wa Miezi 9 alipokuwa na Chelsea na kufukuzwa Mwezi Machi Mwaka huu, Villas-Boas amekiri zama za sasa haiwezekani Meneja akawa na himaya ndefu kama vile Sir Alex Ferguson na Manchester United na Arsene Wenger na Arsenal.
Villas-Boas amesema: “Kwa sasa hilo haliwezekani! Nilitegemea Rafa Benitez atapata himaya ndefu Liverpool lakini haikutokea [Alifukuzwa baada ya Miaka 6]”
Alimalizia: “Ni ngumu Nchi hii! David Moyes wa Everton anakaribia historia hiyo lakini huwezi kupata mifano mingi kama hiyo.” na tano juma

No comments:

Post a Comment