
Rais wa
Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), Aman Ibrahim Makungu alisema jana kwamba, hadi jana wamepata kiasi hicho tu cha fedha
kutokana na viingilio.
Aidha,
Makungu amesema wadhamini wa michuano hiyo wamechangia kiasi cha Sh. Milioni 67
na kwamba hiyo ndiyo siri ya kufanikiwa kwa mashindano ya mwaka huu ya Kombe la
Mapinduzi.
Mapato hayo
yanatokana na jumla ya mechi 15 za mashindano ya mwaka huu hadi fainali jana,
kuanzia hatua ya makundi. Timu nane zilishiriki mashindano haya, ambazo ni
Simba SC ya Dar es Salaam, Tusker FC ya Kenya, Bandari ya Unguja na Jamhuri ya
Pemba zilizokuwa Kundi A, Azam FC ya Dar es Salaam, Mtibwa Sugar ya Morogoro,
Coastal Union ya Tanga na Miembeni ya Unguja zilizokuwa Kundi B.
Kutoka Kundi
A, Tusker walifuzu kama vinara, wakati Simba SC walifuzu kama washindi wa pili
na Kundi B Azam FC walifuzu kama washindi wa kwanza na Miembeni washindi wa
pili. Katika Nusu Fainali, Azam iliitoa Simba SC kwa penalti 5-4 kufuatia sare
ya 2-2 ndani ya dakika 120, wakati Tusker walitumia dakika 90 kuibanjua
Miembeni 2-0.
Azam FC jana
usiku walitetea Kombe la Mapinduzi kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar baada ya
kuifunga Tusker FC ya Kenya mabao 2-1.

Katika
mchezo huo uliochezeshwa na refa Ramadhan Rajab Ibada ‘Kibo’ aliyesaidiwa na
Mwanahija Makame Mfumo na Mgaza Kindundi, hadi mapumziko hakuna timu
iliyofanikiwa kupata bao.
Azam ndio
walioshambulia zaidi katika kipindi hicho, lakini hawakuwa na bahati ya kufunga
bao japo moja. Gaudence Mwaikimba alipewa pasi nzuri na Brian Umony dakika ya
44, lakini shuti lake kali lilidakwa na kipa Samuel Odhiambo.
Kipindi cha
pili, Tusker walirudi na moto mkali na kuanza kusukuma mashambulizi mfululizo
langoni mwa Azam.
Hiyo
iliwasaidia mabingwa hao wa Kenya kupata bao dakika ya 60, lililofungwa na
Jesse Were aliyeunganisha kwa shuti kali la kimo cha mbuzi pasi ya Robert
Omunok.
Hata hivyo,
bao hilo halikudumu sana, kwani Azam FC walisawazisha dakika ya 72 lililofungwa
kwa mkwaju wa penalti na beki Mkenya, Joackins Atudo baada ya beki wa Tusker,
Luke Ochieng kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.
Katika
dakika mbili za nyongeza baada ya kutimu kwa dakika 90 za mchezo huo,
alijitokeza binti mwenye umri kati ya 14 na 16 na kukatiza uwanjani akitokea
jukwaa la Urusi.
Refa
alijaribu kumsimamisha, lakini aliendelea kukatiza Uwanja hadi nje ambako
alipokewa na askari Polisi na kutolewa nje kabisa ya Uwanja. Mtangazaji wa Uwanja
wa Amaan, Farouk Karim aliwatuliza mashabiki akisema binti huyo ametoroka
hospitali ya vichaa, Kidongo Chekundu na tayari Polisi wamemkamata na
kumrejesha huko.
Hadi dakika
90 zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1 na ndipo zikaongezwa
dakika 30.
Gaudence
Exavery Mwaikimba aliipatia Azam bao la ushindi dakika ya pili tu tangu kuanza kwa
muda wa nyongeza baada ya kuwazidi nguvu na maarifa mabeki wa Tusker.
Aidha, Jesse
Were mshambuliaji wa Tusker aliibuka mfungaji bora kwa mabao yake matano na
kuzawadiwa Sh. 300,000, akifuatiwa na Joackins Atudo wa Azam aliyefunga mabao
matatu sawa na Adeyum Saleh Ahmed wa Miembeni.
WAFUNGAJI WA MABAO:
Jesse Were Tusker FC 5
Joackins
Atudo Azam FC 3
Adeyum
Saleh Miembeni
3
Gaudence
Mwaikimba Azam FC 2
Haruna
Chanongo Simba SC 2
Mfanyeje
Mussa Jamhuri 2
Michael Olunga Tusker FC 2
MATOKEO YA MECHI ZOTE KOMBE LA
MAPINDUZI 2013:
Janauri 2, 2013
Tusker 5-1
Bandari
Simba SC 2-2
Jamhuri
Januari 3, 2013
Mtibwa Sugar
1-4 Miembeni
Azam FC 0-0
Coastal Union
Januari 4, 2013
Jamhuri 2-1
Bandari
Simba SC 1-1
Tusker FC
Januari 5, 2013
Mtibwa Sugar
1-1 Coastal Union
Miembeni 1-2
Azam
Januari 6, 2013
Tusker 1-0
Jamhuri
Simba SC 1-1
Bandari
Januari 7, 2013
Miembeni 0-0
Coastal Union
Azam FC 0-0
Mtibwa Sugar
Januari 9, 2013; NUSU FAINALI
Azam FC 2-2
Simba SC (penalti 5-4)
Januari 10, 2013; NUSU FAINALI
Tusker FC
2-0 Miembeni FC
Januari 12, 2013; FAINALI
Azam FC 2-1
Tusker FC
ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI
2003 Mtibwa Sugar
2004 Yanga SC
2005 Yanga SC
2006 Simba SC
2007 Yanga SC
2008 Simba SC
2009 Miembeni FC
2010 Mtibwa Sugar
2011 Simba SC
2012 Azam FC
2013 Azam FC
No comments:
Post a Comment