Tuesday, January 22, 2013

KAGERA SUGAR ASHINDWA KUTAMBA MBELE YA MAAFANDE WA TABORA POLISI TABORA ALLY HASSAN MWINYI.


Timu ya kagera sugar kutoka katika mashamba ya miwa bukoba kule leo imeshindwa kutamba mbele ya wapiga kwata wa mkoani tabora polisi tabora baada ya kufungana bao 1-1 mchezo wa mwisho wa ziara wa kagera sugar ambayo ilikuwa tabora ikitoka burundi ilikokuwa imeenda kucheza mechi za kirafiki.

Kama kawaida timu ya wakatamiwa kagera sugar walikuwa wa kwanza kujipatia bao lao kupitia kwa mshambuliaji wao kutoka nigeria Wilfredy Emme aliyewachambua mabeki wa polisi tabora na kuachia shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa polisi tabora Abdul Aziz.

Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza timu ya kagera sugar walienda mbele kwa bao lao 1-0 kama jana ilivyokuwa kwa rhino rangers na kipindi cha pili timu ya maafande wa polisi tabora walirudi wakiwa wamerekebisha makosa yao.

Na mnamo dakika ya 57 daniel msengi aliunganisha krosi vizuri iliyochongwa na mshambuliaji w atimu hiyo iddy kibwana na kufanya matokeo kuwa 1-1.Hadi dakika 90 za mchezo mwamuzi anapuliza kipenga cha mwisho timu zote zilitoka hakuna mbabe baada ya kutoshana nguvu ya bao moja kwa moja 1-1.

Na kesho katika dimba hilo hilo la ALLY HASSAN MWINYI kutakuwa na mpambano mwingine wa kirafiki kati ya wanakisha mapanda wa mwanza toto african dhidi ya wanajeshi wa hapa mkoani tabora rhino rangers mchezo wa kujipima nguvu kuelekea katika duru la pili la ligi kuu tanzania VPL na ligi daraja la kwanza tanzania FDL ammbapo michuano hiyo inatarajia kuanza kutimua vumbi jan 26.1.2013 katika viwanja tofauti hapa tanzania.

Mchezo wa leo umeingiza shilingi laki nane na elfu hamsini na nane 858,000 kutokana na mashabiki mia nane na hamsini na nane 858 waliokata tiketi kuangalia mchezo huu kwa shilingi 1000 ikumbukwe jana waliingia watazamaji 1630 na kupata shilingi mil.1630000 kuangalia mechi ya rhino rangers na kagera sugar.
Leo wachezaji wa

KAGERA SUGAR+Andrew ntala,luhende kanyata,martin muganyizi,lamban kambole,malegesi mwangwa,zubery dabi,mecky maiko,shamte odiro,shija mkina,paul ngwai,
walioingia kipindi cha pili ni adam oseja,juma nade,benjamin asukile,george kavilla,daudi jumanne,rashid madawa,paul kabange na kamana salum.
POLISI TABORA+Abdul aziz,kaizar kilowoko,josephy manyira,jeremia ng'ambi,jamali jumanne,benard adam,mussa boaz,hussein abdalah,ramadhan semwa,daniel msengi na iddy kibwana.
BECHI+husein abdalah,david joseph,ibrahim mussa,baraka adim,ernest nkadi,na john matuli.

No comments:

Post a Comment