Wednesday, January 23, 2013

IVORY COAST YAIBANJUA TOGO 2-1,GERVINHO AITAKATIISHA IVORY


Ivory Coast imeanza kampeini yake ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika kwa kuilaza Togo kwa magoli mawili kwa moja katika mechi yao ya ufunguzi ya Kundi D.
Ivory Coast ilipata bao lake la kwanza kunako dakika ya nane kupitia kwa mchezaji Yaya Toure na kwa mara nyingine, wachezaji hao wa Ivory Coast wanatafuta fursa ya kutwaa kombe hilo ambalo liliwaponyoka mwaka uliopita.Nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba, analiongoza tena timu hiyo, kwa fainali hizo ambazo ndizo za mwisho atakazoshiriki. Licha ya wengi kuipa timu hiyo ya Ivory Coast nafasi kubwa ya kushinda mashindano ya mwaka huu, The Elephants hawakucheza mechi ya kusisimua katika kipindi cha kwanza.
Mara ya Mwisho Ivory Coast, ilishinda kombe hilo ni mwaka wa 1992.



Togo nayo inaongozwa na mshambulizi wa Tottenham, Emmanuel Adebayor.
Dakika ya 44, Yahya Toure, nusura afunge bao la pili, lakini mkwaju wake uligonga mlingoti.
Ushirikiano kati ya Didier Drogba, Yahya Toure and Gervinho umeonekana kuwa nguzo ya timu hiyo ya Ivory Coast.
Dakika moja baadaye Togo ikasawazisha baada ya walinda lango wa Ivory Coast kufanya masihara, kwenye eneo la hatari.
Kufikia wakati wa mapumziko timu hizo mbili zilikuwa zikitoshana na nguvu ya kufungana bao moja kwa moja.
Lakini katika kipindi cha pili, Ivory Coast iliimarisha mashambulizi yake na kunako dakika ya 87, ivory coast ikapata bao lake la pili kupitia kwa mchezaji Gervinho.
Ivory Coast sasa inaongoza kundi hilo la alama tatu huku Togo ikiwa bila alama yoyote.
Kinyume na ilivyotarajiwa, mechi hiyo iligeuka na kuwa maonyesho ya nguvu, baina ya wachezaji kadhaa wanaoshiriki katika ligi mbali mbali za kulipwa na mara nyingi ilikuwa kati ya Kolo Toure na Adebayor na Vincent Bossou na Didier Drogba ambao walifanya makosa mengi na hivyo kuhujumu mtiririko wa mechi hiyo.
Mechi ya pili ya kundi hilo kati ya Tunisia na Algeria itaanza mwendo wa saa tatu za usiku majira ya Afrika Mashariki.

Gervinho akishangilia kivyake baada ya kuiokoa Ivory Coast usiku huu.
Vinara wa EPL Kolo Toure (kushoto), Cheick Tiote (kulia) na Emmanuel Adebayor (kati) wakigombea mpira usiku huu kwenye AFCON 2013

Yaya Toure (katikati) akipongezwa na wenzake

Gervinho akishangilia baada ya kuifungia timu yake goli la ushindi na hapa anabusu uzi

Shabiki wa Togo kushoto na kulia ni shabiki wa Ivory Coast akipuliza "vuvuzela"

MSIMAMO:
[Kila Timu imecheza Mechi 1]
KUNDI A
-South Africa Pointi 1
-Cape Verde 1
-Morocco 1
-Angola 1
KUNDI B
-Mali Pointi 3
-Congo DR 1
-Ghana 1
-Niger 0
KUNDI C
-Burkina Faso Pointi 1
-Ethiopia 1
-Nigeria 1
-Zambia 1
KUNDI D
-Ivory Coast Pointi 3
-Tunisia 3
-Togo 0
-Algeria 0
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA/MATOKEO:
[SAA za BONGO]
Jumamosi Januari 19
South Africa 0 Cape Verde Islands 0
Angola 0 Morocco 0
Jumapili Januari 20
Ghana 2 Congo DR 2
Mali 1 Niger 0
Jumatatu Januari 21
Zambia 1 Ethiopia 1
Nigeria 1 Burkina Faso 1
Jumanne Januari 22
Ivory Coast 2 Togo 1
Tunisia 1 Algeria 0
Jumatano Januari 23
South Africa v Angola [Moses Mabhida Stadium Saa 12 Jioni]
Morocco v Cape Verde Islands [Moses Mabhida Stadium Saa 3 Usiku]
Alhamisi Januari 24
Ghana v Mali [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 12 Jioni]
Niger v Congo DR [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 3 Usiku]
Ijumaa Januari 25
Zambia v Nigeria [Mbombela Stadium Saa 12 Jioni]
Burkina Faso v Ethiopia [Mbombela Stadium Saa 3 Usiku]
Jumamosi Januari 26
Ivory Coast v Tunisia [Royal Bafokeng Stadium Saa 12 Jioni]
Algeria v Togo [Royal Bafokeng Stadium Saa 3 Usiku]
Jumapili Januari 27
Morocco v South Africa [Moses Mabhida Stadium Saa 2 Usiku]
Cape Verde Islands v Angola [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 2 Usiku]
Jumatatu Januari 28
Congo DR v Mali [Moses Mabhida Stadium Saa 2 Usiku]
Niger v Ghana [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 2 Usiku]
Jumanne Januari 29
Ethiopia v Nigeria [Royal Bafokeng Stadium Saa 2 Usiku]
Burkina Faso v Zambia [Mbombela Stadium Saa 2 Usiku]
Jumatano Januari 30
Algeria v Ivory Coast [Royal Bafokeng Stadium Saa 2 Usiku]
Togo v Tunisia [Mbombela Stadium Saa 2 Usiku]
ROBO FAINALI
Jumamosi Februari 2
Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B [Moses Mabhida Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
Jumapili Februari 3
Mshindi Kundi D v Mshindi wa Pili Kundi C [Royal Bafokeng Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi Kundi C v Mshindi wa Pili Kundi D [Mbombela Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
NUSU FAINALI
Jumatano Februari 6
Mshindi RF 3 v Mshindi RF 2 [Mbombela Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi RF 1 v Mshindi RF 4 [Moses Mabhida Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
MSHINDI wa TATU
Jumamosi Februari 9
[Nelson Mandela Bay Stadium Saa 3 Usiku]
FAINALI
Jumapili Februari 10
[Soccer City Saa 3 Usiku]

No comments:

Post a Comment