Saturday, January 26, 2013

BAADA YA VIJANA WA SIMBA KUFUNGWA NA VIBONDE WA SOUTH JUZI LEO SIMBA YAUA KWA SUMU YA OMAN, AZAM NAYO MOTO ULE ULE KWELI LIGI MSIMU HUU NI BALAA





SIMBA SC leo imeanza vyema mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuichapa mabao 3-1 African Lyon ya Dar es Salaam katika mchezo wa ufunguzi wa duru hilo.
Ushindi huo, unaifanya  
Hadi mapumziko Simba SC walioweka kambi ya wiki mbili Oman kujiandaa na mzunguko huu, tayari walikuwa mbele kwa mabao 3-0, yaliyotiwa kimiani na Mrisho Khalfan Ngassa mawili dakika za 19 na 39 na Ramadhan Suleiman Chombo ‘Redondo’ dakika ya tatu ya mchezo huo.
Redondo aliifungia Simba SC bao la kwanza dakika ya tatu, akiunganisha krosi nzuri ya Ngassa kutoka wingi ya kushoto na kufumua shuti akiwa katikati ya msitu wa mabeki wa Lyon.
Bao hilo liliwatia chaji Simba SC na kuanza kucheza soka maridadi zaidi, wakionana kwa pasi za mitindo yote, ndefu, fupi, za juu, chini hadi visigino na haikushangaza dakika ya 19 walipopata bao la pili.
Ilikuwa ni kazi nzuri ya Ngassa mwenyewe, ambaye baada ya kupata pasi ya Mwinyi Kazimoto Mwitula aliitoka ngome ya Lyon kabla ya kumchambnua kipa wa timu hiyo, Abdul Seif.
Baada ya kufunga bao hilo, Ngassa alikwenda moja kwa moja kwenye benchi la wachezaji wa akiba na kukumbatiana na Haruna Moshi Shaaban ‘Boban’ kisha kuwapa mikono wachezaji kadhaa na kurejea uwanjani.
Lyon walipoteza nafasi nzuri ya kupata bao dakika ya 31, baada ya Shamte Ally Kilalile kukosa penalti.
Refa Israel Mujuni alitoa penalti hiyo baada ya beki Paul Ngalema kumkwatua beki Fred Lewis aliyepanda kusaidia mashambulizi, hata hivyo mkwaju wa kwanza wa Shamte ulipanguliwa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja, lakini mwamuzi akaamuru irudiwe kwa madai kipa huyo alitokea kabla ya mpira kupigwa na safari hiyo mpigaji akapiga nje kabisa.
Simba iliongeza kasi ya mashambulizi ikitumia mipira ya pembeni, kulia akiteleza Chanongo na kushoto Ngassa, timu ikichezeshwa vyema na viungo watatu katikati, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto na Jonas Mkude. Ilikuwa burudani kwa mashabiki wa Wekundu hao wa Msimbazi, kwa jinsi ambayo timu yao ilitawala mchezo.
Kazi nzuri ya Chanongo aliyeteleza wingi ya kulia huku akiruka madaluga ya mabeki wa Lyon, iliipatia Simba bao la tatu baada ya krosi yake nzuri kuunganishwa vyema kimiani na Ngassa.  
Baada ya kufunga, Ngassa alishangilia kwa aina yake bao hilo, kwanza akitambaa hadi langoni na kisha kujilaza kwenye nyavu kubwa kama yeye ndio mpira.
Baada ya hapo, aliinuka na moja kwa moja kwenda tena kwenye benchi la wachezaji wa akiba akianza kushangilia na Boban, baadaye wachezaji wengine na kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, ambaye alitumia kama sekunde 30 akizungumza naye jambo.  
Kipindi cha pili, Lyon walibadilika na kuwabana Simba SC wasiongeze mabao zaidi, huku wao wakifanikiwa kupata bao la kufutia machozi, lililofungwa na Bright Ike dakika ya 59, pasi ya Fred Lewis.
Katika mechi nyingine, Mtibwa Sugar ililala 1-0 nyumbani mbele ya Polisi Morogoro, Coastal Union iliifunga Mgambo JKT 3-1, Ruvu Shooting iliilaza 1-0 JKT Ruvu, Azam FC imeshidna 3-1 dhidi ya Kagera Sugar na JKT Oljoro imeilaza 3-1 Toto Africans.
Ligi hiyo itaendelea kesho wakati vinara, Yanga SC watakapomenyana na TZ Prisons kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba SC; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Paul Ngalema/Kiggi Makassy, Mussa Mudde/Komabil Keita, Shomary Kapombe, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto, Haruna Chanongo, Mrisho Ngassa/Abdallah Seseme, Amri Kiemba na Ramadhan Chombo ‘Redondo’.
African Lyon; Abdul Seif, Fred Lewis, Jacob Massawe, Mohamed Samatta, Abdulaghan Gulam/Hood Mayanja, Yussuf Mlipili, Jackson Kanywa, Aman Kyata/Yussuf Mgwao, Job Ibrahim, Shamte Ally/Bright Ike na Juma Seif ‘Kijiko’.
MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM 2012/2103:   
                                P    W  D   L    GF GA GD Pts
1    Yanga                13 9    2    2    25 10 15 29
2    Azam                 14 8    3    3    20 12 8    27
3    Simba SC           14 7    5    2    23 12 11 26
4    Mtibwa Sugar     14 6    4    4    18 13 5    22
5    Coastal Union    14 7    4    3    19 15 4    25
6    Kagera Sugar     14 5    6    3    16 13 3    21
7    Ruvu Shooting   14 7    2    5    20 17 3    23
8    Mgambo JKT      14 5    2    7    11 16 -5  17
9    JKT Ruvu            14 4    3    7    13 21 -8  15
10 JKT Oljoro           14 5    5    5    16 17 -1  17
11 TZ Prisons           13 3    5    5    8    12 -4  14
12 Toto African         14 2    6    6    11 18 -7  12
13 African Lyon         14 2    3    9    10 23 -13 9
14 Polisi Moro           14 1    4    9    5    16 -11 7
MATOKEO KAMILI MECHI ZA LEO:
Mtibwa Sugar 0-1 Polisi Morogoro
Coastal Union 3-1 Mgambo JKT
Ruvu Shooting 1-0 JKT RUVU
Azam FC 3-1 Kagera Sugar
JKT Oljoro 3-1 Toto Africans
KESHO; Januari 27, 2013
Yanga SC Vs TZ Prisons

No comments:

Post a Comment