Thursday, November 15, 2012


JOSEPH OWINO NJIANI KURUDI NYUMBANI MSIMBAZI

Zoezi la klabu bingwa ya Tanzania bara Simba kupata mbadala wa beki wake aliyetimkia Yanga, Kelvin Yondani linaendelea, baada ya Lino Musombo kutemwa na kusajiliwa kwa Keita na Ocheing ambao wameonekana kuhangaika kuziba pengo la Yondani, sasa klabu hiyo ya Simba inasemekana wapo katika harakati za kumrudisha moja wa mabeki wao bora katika kipindi cha miaka 10 iliyopita mganda Joseph Owino.

Simba ambao walianza ligi vizuri na kuongoza ligi kwa muda mrefu kabla ya kupoteza muelekeo mwishoni mwa mwa raundi ya kwanza ya msimu wa VPL. Sasa katika kujaribu kuimarisha safu ya ulinzi ya timu hiyo ambayo imeonekana kuyumba sana msimu huu, uongozi wa Simba umeona bora ufanye mpango wa kumrudisha kundini Owino ambaye amesajiliwa Azam lakini amekuwa akikosa namba ya kudumu baada ya kurudi kutoka kwenye majeruhi yaliyomuweka nje kwa muda mrefu.

Taarifa ambazo hazijathibitishwa ni kwamba Simba tayari wapo kwenye mazungumzo na Azam ili kuweza kuona uwezekano wa kumsaini Owino.

Owino ambaye aliondoka Simba baada ya kupata majeraha ya goti ambayo yalimuweka nje kwa muda mrefu, na Azam wakamsajili akiwa mgonjwa wakamtibu lakini baada ya kupona amekuwa na urafiki mzuri na benchi la Chamazi.

 

MICHELSEN AHOFIA WAKONGO KULETA VIJEBA

Michelsen wa tatu kutoka kulia waliosimama akizungumza na wachezaji wa Serengeti. Kulia kwake ni wasaidizi wake, Jamhuri KIhwelo na Manyika Peter, wakati kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Serengeti, Kassim Dewji, Katibu wa Kamati, Henry Tandau, Suleiman na Nyambui na Katibu wa TFF, Angetile Osiah.

KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, Mdenmark Jacob Michelsen amesema kwamba kuelekea mechi ya keshokutwa ana wasiwasi wapinzani wake, Kongo Brazzaville wana wachezaji waliozidi umri.
Akizungumza  jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam baada ya mazoezi ya jioni, Michelsen alisema kwamba ameichunguza vizuri Kongo na sasa anaifahahamu vema.
Serengeti itamenyana na Kongo keshokutwa Uwanja wa Taifa, katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Tatu na ya mwisho ya kuwania kucheza Fainali za Vijana Afrika zitakazofanyika nchini Morocco mwakani.
Michelsen alisema kwamba alikwenda kushuhudia mchezo wa kwanza wa raundi iliyopita, baina ya Kongo na Zimbabwe waliotolewa na wapinzani wao hao na kujionea makali ya wapinzani wao.
Pamoja na kukiri kwamba Kongo ni timu bora na ilicheza Fainali zilizopita za Kombe la Dunia nchini Mexico mwaka jana na kutolewa raundi ya pili, Michelsen alisema bado ana wasiwasi timu hiyo ina ‘vijeba’.
“Nilipokwenda kuwaangalia wakicheza na Zimbabwe, nilikuta kikosini mwao kuna wachezaji sita wa kikosi kilichokwenda Mexico kwenye Kombe la Dunia, inanitia shaka kwa sababu hakuna mchezaji anayeweza kucheza michuano mikubwa kama ile akiwa ana umri wa miaka 15.
Mimi ni kocha wa vijana na ninajua, haiwezekani. Ucheze fainali za Kombe la Dunia za U17 una miaka 15, hakuna,”alisema Michelsen, ambaye aliwataja baadhi ya wachezaji anaowatilia shaka wamezidi umri ni Hady Binguila na Charvely Mabiat.
Pamoja na hayo, Michelsen amesema ana matumaini ya kuwatoa Kongo kutokana na maandalizi yao ya muda mrefu na pia sapoti anayoipata kutoka kwa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Kamati maalum iliyoundwa kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri.
Amesema wamecheza mechi za kujipima nguvu 15 zikiwemo dhidi ya timu za Ligi Kuu na hawajafungwa hata moja, kitu ambacho anaamini ni kipimo cha ubora wa timu yake.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Saidia Serengeti Ishinde, Kassim Dewji alisema kwamba wanapambana kwa uwezo wao wote kuhakikisha timu hiyo inakwenda kwenye fainali za Morocco, mwakani.
Dewji aliwataka wachezaji wa timu hiyo kucheza kwa nidhamu, kujituma na kufuata maelekezo ya makocha wao, ili wapate ushindi katika mchezo wa Jumapili.
Serengeti imefanikiwa kufuzu hadi Raundi ya Tatu bila jasho, baada ya wapinzani wake wa awali katika Raundi ya Kwanza na ya Pili, Kenya na Misri kujitoa. Iwapo timu hii itafuzu, hii itakuwa mara ya pili kwa Serengeti kukata tiketi ya kucheza fainali hizo, baada ya mwaka 2005.
Hata hivyo, pamoja na kuzitoa Rwanda, Zambia na Zimbabwe, Serengeti haikwenda Gambia mwaka huo kutokana na kuondolewa kwenye michuano hiyo na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), baada ya kubainika walitumia kijana aliyezidi umri, Nurdin Bakari.

 

Cisse kuzuiwa na Senegal kuichezea Newcastle?? Suarez kung’oka Anfield??


SUAREZ_V_EVRA12Kukiwa kumezuka mzozo kati ya Senegal na Newcastle kuhusu Straika Papiss Cisse baada ya juzi kutojiunga na Timu ya Taifa ambao unaweza ukaifanya Senagal itumie Sheria ya FIFA na kumfungia Siku 5 ambapo kutamfanya aikose Mechi kati ya Newcastle na Swansea, huko Anfield Liverpool wanahaha kuzima stori zilizoibuka kuwa Straika wao Luis Suarez yuko mbioni kuhamia Manchester City Mwezi Januari Dirisha la Uhamisho likifunguka.
Papiss Cisse could kuikosa Newcastle v Swansea??
Bosi wa Newcastle Alan Pardew ametoboa kuwa Papiss Cisse huenda asicheze Mechi ya Ligi Kuu Jumamosi dhidi ya Swansea kwa sababu ya mgogoro na Senegal kufuatia Straika huyo kutojiunga na Timu ya Taifa ya Senegal ambayo Jumatano, Siku ya Kalenda ya FIFA, ilicheza Mechi ya Kirafiki na Niger.
Inadaiwa sasa Senegal wametishia kuitumia Sheria ya FIFA ya kumfungia Papiss Cisse kwa Siku 5 kwa sababu hawakujulishwa kuhusu Mchezaji huyo kutojiunga na Timu ya Taifa.
Pardew amedai Cisse alikuwa na maumivu ya mgongo aliyoyapata kwenye Mechi ya Jumapili iliyopita waliyofungwa 1-0 na West Ham ambayo yalimlazimu Mchezaji huyo kutolewa nje kwenye Mechi hiyo.
Newcastle imedai ilituma Ripoti ya Madaktari kuhusu Cisse kwa Barua Pepe kwa Chama cha Soka cha Senegal lakini Pardew amesema inaelekea haikupokelewa.
Ikiwa Cisse, Miaka 27, ataikosa Mechi na Swansea hilo litakuwa pigo kwa Newcastle ambao wanahitaji ushindi kwa vile wameshinda Mechi moja tu kati ya sita zilizopita za kwenye Ligi.
Pardew amesema kuwa wanawasiliana na FA ya England na Viongozi wa Senegal ili kupata uhakika kama wanaweza kumtumia Mchezaji huyo Jumamosi.
Luis Suarez ni furaha kubakia Liverpool Miaka mingi!!
Straika wa Liverpool Luis Suarez amesema anafurahia kubakia Liverpool na anataka awe hapo kwa Miaka mingi ingawa sasa kuna tetesi kubwa Manchester City wanataka kumsaini Mwezi Januari Dirisha la Uhamisho likifunguliwa.
Mwanzoni mwa Msimu huu, Suarez alisaini Mkataba mpya na Liverpool na Msimu huu amekuwa kwenye fomu nzuri kwa kufunga Mabao 11 katika Mechi 16 alizochezea Liverpool.
++++++++++++++++++++++++++
Luis Suarez akiwa Liverpool
-ALISAINIWA: Januari 2011 (£22.7m)
-MECHI: 68
-MAGOLI: 32
++++++++++++++++++++++++++
Hata hivyo, Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers, amesema Mchezaji huyo hauzwi.
Rodgers ametamka: “Tukimpoteza Suarez hatuna Straika, hivyo hatuwezi kumuuza.”
Tangu atue England Suarez, licha ya kufanya vizuri akiwa na Liverpool, amekuwa akikumbwa na migogoro ya mara kwa mara.
Alifungiwa Mechi 8 baada ya kumkashifu Kibaguzi Beki wa Manchester United Patrice Evra na baada ya hapo akazua mzozo mpya baada ya kukataa kumpa mkono Evra Timu za Liverpool na Man United zilipokutana Old Trafford.
Hata hivyo, Msimu huu, Wachezaji hao walipeana mikono Timu zao zilipokutana.
Hivi karibuni aliandamwa kwa madai kuwa hujiangusha makusudi kwenye Eneo la Penati ili kuwahadaa Marefa apewe Penati tabia ambayo wakati mwingine imemdhuru mwenyewe kwa kunyimwa Penati za wazi huku Marefa wakidhani anawadaa.



DABI ya LONDON Jumamosi: AVB adai Spurs ni lazima wawe juu ya Arsenal!! 
>>AVB akata tamaa Ubingwa, ataka nafasi ya 4 tu!!
>>AKIRI BINGWA Ni Man United, City au Chelsea, walobaki kugombea 4!
AVB_ACHUCHUMAAIli kuishika nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England ili wapate fursa ya kucheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI, Andre Villas-Boas anaamini Tottenham ni lazima wamalize Ligi wakiwa juu ya Arsenal Msimu huu.
Lakini mara ya mwisho kwa Tottenham kumaliza Ligi wakiwa mbele ya Arsenal ni Mwaka 1995 wakati hata Arsene Wenger, Meneja wa sasa wa Arsenal, hajaanza kibarua.
Msimamo huo wa Villas-Boas umetolewa kwenye mahojiano na Wanahabari kuhusu Dabi yao na Arsenal itakayochezwa Jumamosi Uwanja wa Emirates.
Villas-Boas alijibu swali kuhusu nini lengo lao Msimu huu kwa kusema: “Ninachoona ni dhahiri Man United, Man City na Chelsea wapo kwenye mbio kubwa za Ubingwa. Ingawa ngumu kumaliza nafasi ya 4 lakini ni lazima tumalize juu ya Arsenal ili kuipata.”
++++++++++++++++++++++++
DONDO za DABI: Arsenal v Tottenham
-Tottenham wamepoteza Mechi moja tu kati ya 5 walizocheza mwisho na Arsenal.
-Magoli 100 yamefungwa katika Dabi 32 tangu Arsene Wenger atue Arsenal
++++++++++++++++++++++++
Kimsimamo, kwa sasa, Tottenham wapo nafasi ya 7 wakiwa Pointi 1 mbele ya Arsenal walio nafasi ya 8.
Tottenham wapo Pointi 7 nyuma ya Timu ya 3 Chelsea na Pointi 10 nyuma ya vinara Manchester United.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
1 Man United Mechi 11 Pointi 27
2 Man City  Mechi 11 Pointi 25
3 Chelsea Mechi 11 Pointi 24
4 Everton Mechi 11 Pointi 20
5 WBA Mechi 11 Pointi 20
6 West Ham Mechi 11 Pointi 18
7 Tottenham Mechi 11 17
8 Arsenal Mechi 11 Pointi 16
+++++++++++++++++++++++
Msimu uliopita Arsenal walimaliza wakiwa nafasi ya 3 na Tottenham nafasi ya 4 lakini Tottenham hawakupewa nafasi ya kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kama ilivyotakiwa kwa vile Chelsea walitwaa Ubingwa wa UEFA CHAMPIONZ LIGI na hivyo kupewa nafasi ya kutetea Taji lao na Tottenham kutupwa kwenye EUROPA LIGI.
Wakati huo huo, Villas Boas amethibitisha Kiungo wa Belgium Mousa Dembele hatacheza Dabi hiyo na Arsenal kwa vila bado ana tatizo la nyonga.
Baada ya kuumia nyonga, Dembele amezikosa Mechi 8 za Tottenham.
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi, Novemba 17, 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Arsenal v Tottenham Hotspur
[SAA 12 Jioni]
Liverpool v Wigan Athletic
Manchester City v Aston Villa
Newcastle United v Swansea City
Queens Park Rangers v Southampton
Reading v Everton
West Bromwich Albion v Chelsea
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Norwich City v Manchester United
Jumapili, Novemba 18, 2012
[SAA 1 Usiku]
Fulham v Sunderland
Jumatatu, Novemba 19, 2012
[SAA 5 Usiku]
WestHam v Stoke City
MAREFA-Ratiba ya Mechi zao:
Jumamosi Novemba 17
Arsenal v Tottenham
Refa: H Webb
Refa Wasaidizi: M Mullarkey,  D Cann
Refa wa Akiba: C Foy
Reading v Everton
Refa: M Atkinson
Refa Wasaidizi: P Kirkup, J Flynn
Refa wa Akiba: A Marriner
West Bromwich Albion v Chelsea
Refa: M Oliver
Refa Wasaidizi: S Child, D England
Refa wa Akiba: S Attwell
Manchester City v Aston Villa
Refa: J Moss
Refa Wasaidizi: S Beck, A Holmes
Refa wa Akiba: L Probert
Newcastle United v Swansea City
Refa: P Dowd
Refa Wasaidizi: A Garratt, S Ledger
Refa wa Akiba: A Bates
Queens Park Rangers v Southampton
Refa: M Dean
Refa Wasaidizi: J Collin, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason
Liverpool v Wigan Athletic
Refa: K Friend
Refa Wasaidizi: R Ganfield, A Halliday
Refa wa Akiba: J Adcock
Norwich City v Manchester United
Refa: A Taylor
Refa Wasaidizi: R West, P Bankes
Refa wa Akiba: N Swarbrick
Jumapili Novemba 18
Fulham v Sunderland
Refa: L Probert
Refa Wasaidizi: D Bryan, L Betts
Refa wa Akiba: A Marriner
Jumatatu Novemba 19
West Ham United v Stoke City
Refa: C Foy
Refa Wasaidizi: H Lennard, M McDonough
Refa wa Akiba: H Webb

BPL: Baada Robo Msimu, Msimamo kufuata Historia, kubaki hivi hivi??

>>KWA MIAKA 20, BAADA Mechi 10, ni mara 3 tu Man United kileleni na mara zote 3 walimaliza Mabingwa!!!
>>FAHAMU MAREFA MECHI ZA WIKENDI HII!
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
1 Man United Mechi 11 Pointi 27
2 Man City  Mechi 11 Pointi 25
3 Chelsea Mechi 11 Pointi 24
4 Everton Mechi 11 Pointi 20
5 WBA Mechi 11 Pointi 20
6 West Ham Mechi 11 Pointi 18
7 Tottenham Mechi 11 17
8 Arsenal Mechi 11 Pointi 16
+++++++++++++++++++++++
FERGIE_MAZOEZINIAkijibu swali mara baada ya kuifunga Manchester United Bao 1-0 katika Wikiendi ya ufunguzi ya MsimuWENGER_AHIMIZA12 huu wa Ligi Kuu England, Meneja wa Everton David Moyes alisema ni mapema kuitathmini Timu yake labda baada ya Mechi 10, msimamo ambao ulichukuliwa pia na Mameneja wa Arsenal, Arsene Wenger, na wa Newcastle, Alan Pardew, na leo hii Timu zimeshacheza Mechi 11, Robo ya Ligi nzima, na Manchester United ndio wako kileleni, hii ikiwa mara yao ya 3 tu kuwa hapo baada ya Mechi 10 ingawa wametwaa Taji mara 12 lakini katika mara zote hizo 3 walizokuwa kileleni wao ndio waliibuka Mabingwa.
Akiongea, Meneja wa zamani wa England, Graham Taylor, alisema: “Msimamo wa Ligi wa Kipindi hiki huwa haubadiliki sana ifikapo Mwezi Mei. Pengine zitatokea Klabu moja au mbili ambazo zitaleta maajabu lakini si zaidi.”
Nae David Pleat, Meneja wa zamani wa Tottenham, amesema: “Baada ya Robo ya Msimu, unapata fununu nini kitaendelea. Klabu mbili za Manchester zipo juu pamoja na Chelsea. Inawezekana Masimu huu Timu ngeni ikakamata nafasi ya 4 ingawa Arsenal na Tottenham hawatakuwa mbali.”
Akiongeza, David Pleat, alisema wasiwasi mkubwa ni ule uwezekano wa Klabu mbili au tatu kufungua pengo kubwa kileleni na pia Klabu za mkiani kuachwa mbali nyuma.
Ingawa kwa wakati huu Msimamo hauleti dira ya kweli nini kitatokea mwishoni mwa Msimu lakini takwimu zinaonyesha katika Miaka 20 Man United, chini ya Sir Alex Ferguson, imetwaa Taji mara 12 na katika mara hizo walikuwa kileleni mara 3 tu baada ya Mechi 10 lakini katika mara zote hizo 3 walimaliza Msimu wakiwa Mabingwa na hilo limemfanya Graham Taylor atamke: “Hiyo ni dalili mbaya kwa Wapinzani wa Man United. Kawaida hawaanzi Ligi vizuri na ni baadae ndio wanakaza uzi lakini sasa wapo juu bila hata kuonekana wamegangamara.”
Mbali ya mbio za Ubingwa na kumaliza kuwa katika Timu 4 bora ili kucheza Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI, pia ipo vita ya kujinusuru kutimuliwa kwa Mameneja wa Timu zinazofanya vibaya na pia ile vita ya kukwepa kuporomoka Daraja.
Wakiwa mkiani, Meneja wa Southampton, Nigel Adkins, amekiri yeye ndie anaeongoza kwa kuwa Meneja wa kwanza kutegemewa kumwaga unga hali ambayo pia inampa presha Mark Hughes, Meneja wa QPR, ambae Timu yake ipo juu tu ya Southampton.
Katika historia ya Ligi Kuu England, Klabu ambayo pia ilifungwa bao nyingi kufikia hatua hii ya Mechi 10 kama ambavyo Southampton imefungwa, Mabao 28, ni Barnsley katika Msimu wa 1997/8 na ikashushwa Daraja.
Graham Taylor amezitambua West Bromwich Albion chini ya Meneja Steve Clarke, ambao wapo nafasi ya 5, Fulham, nafasi ya 8 na Wigan, nafasi ya 13, kuwa ndizo Timu zinazostahili pongezi kwa mafanikio yao kufikia hatua hii ya Mechi 10.
Pamoja na hizo pia aliipa mkono Everton kwa wanzo mwema ambapo sasa wapo nafasi ya 4.
Akiizungumzia Wigan, ambayo katika hatua hii Msimu uliopita ilikuwa mkiani na hatimae kujikokota na kujinusuru na kumaliza ikiwa nafasi ya 15, David Pleat amesema: “Timu zinazosuasua hubadilisha Mameneja, hubadilisha Wachezaji kwenye Dirisha la Uhamisho, lakini Wigan hawakufanya hata moja kati ya hayo! Meneja Roberto Martinez alibadilisha Mfumo wa Uchezaji na hilo limeleta mafanikio makubwa! Huu ni mfano mzuri wa kuigwa na wengine!”
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi, Novemba 17, 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Arsenal v Tottenham Hotspur
[SAA 12 Jioni]
Liverpool v Wigan Athletic
Manchester City v Aston Villa
Newcastle United v Swansea City
Queens Park Rangers v Southampton
Reading v Everton
West Bromwich Albion v Chelsea
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Norwich City v Manchester United
Jumapili, Novemba 18, 2012
[SAA 1 Usiku]
Fulham v Sunderland
Jumatatu, Novemba 19, 2012
[SAA 5 Usiku]
WestHam v Stoke City
MAREFA-Ratiba ya Mechi zao:
Jumamosi Novemba 17
Arsenal v Tottenham
Refa: H Webb
Refa Wasaidizi: M Mullarkey,  D Cann
Refa wa Akiba: C Foy
Reading v Everton
Refa: M Atkinson
Refa Wasaidizi: P Kirkup, J Flynn
Refa wa Akiba: A Marriner
West Bromwich Albion v Chelsea
Refa: M Oliver
Refa Wasaidizi: S Child, D England
Refa wa Akiba: S Attwell
Manchester City v Aston Villa
Refa: J Moss
Refa Wasaidizi: S Beck, A Holmes
Refa wa Akiba: L Probert
Newcastle United v Swansea City
Refa: P Dowd
Refa Wasaidizi: A Garratt, S Ledger
Refa wa Akiba: A Bates
Queens Park Rangers v Southampton
Refa: M Dean
Refa Wasaidizi: J Collin, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason
Liverpool v Wigan Athletic
Refa: K Friend
Refa Wasaidizi: R Ganfield, A Halliday
Refa wa Akiba: J Adcock
Norwich City v Manchester United
Refa: A Taylor
Refa Wasaidizi: R West, P Bankes
Refa wa Akiba: N Swarbrick
Jumapili Novemba 18
Fulham v Sunderland
Refa: L Probert
Refa Wasaidizi: D Bryan, L Betts
Refa wa Akiba: A Marriner
Jumatatu Novemba 19
West Ham United v Stoke City
Refa: C Foy
Refa Wasaidizi: H Lennard, M McDonough
Refa wa Akiba: H Webb

No comments:

Post a Comment